MAKOMANDOO YANGA WAJIKOMBA KWA AL-MASRY, WAOMBA JEZI , WAAMBULIA PATUPU>> - LAKE MEDIA TV

Breaking

Music

BANNER 728X90

Wednesday, 7 March 2018

MAKOMANDOO YANGA WAJIKOMBA KWA AL-MASRY, WAOMBA JEZI , WAAMBULIA PATUPU>>

BAADHI YA MASHABIKI WA YANGA KATIKA MOJA YA MECHI ZA LIGI KUU BARA WAKIWA WAMEPENDEZA KATIKA JEZI ZA TIMU HIYO UKIACHANA NA WALE WAPUUZI WACHACHE WALIOKWENDA KUJIPENDEKEZA NA KUOMBA JEZI ZA WAARABU WA AL MASRY.



Hii ni sura mbaya na ya kushangaza.

Juzi Jumatatu, baadhi ya makomandoo wa Yanga na mashabiki waliamua kuvamia mazoezi ya Al Masry na kuomba jezi ili waweze kuishangilia timu hiyo katika mchezo wa dhidi ya Simba, huku wakisikika wakisema ‘Simba 1 Al Masry 3’.

Katika mchezo huo ambao unapigwa leo Jumatano saa 12 jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, makomandoo hao hawakusita kuonyesha ushabiki wao kwa timu hiyo wakati wakifanya mazoezi juzi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam huku wakilitaja jina la mshambuliaji wa timu hiyo,  Aristide Bance raia wa Burkinafaso.

Makomandoo hao walifika uwanjani hapo kuangalia mazoezi ya wapinzani wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Township Rollers kabla ya  mchezo wao uliopigwa jana kwenye Uwanja wa huo ambapo timu hiyo ilipomaliza mazoezi na kuwapisha Al Masry, wao walikomaa na kuwafuata viongozi ili wawape jezi watakavaa leo na kuwashangilia.

Tuliwashuhusia makomandoo hao wakijadiliana kuwaomba jezi viongozi hao  kabla ya kuwafuata  lakini hawakuweza kufanikiwa kwa kuwa wajibiwa kuwa:” Mtatusamehe, hatujabeba jezi za kutosha.”


“Lazima Simba itafungwa mabao 3-1, nawahakikishia na wale msiwe na hofu hata kidogo,” alisema shabiki mmoja akiwa amevaa jezi ya Yanga wakati anahojiwa na kituo kwa One Sport cha Misri.

SOURCE: CHAMPIONI

No comments:

Post a Comment